Isaiah 63:1-6

Siku Ya Mungu Ya Kisasi Na Ukombozi


1 aNi nani huyu anayekuja kutoka Edomu,
kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu?
Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari,
anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake?

“Mimi ndimi, nisemaye katika haki,
mwenye nguvu wa kuokoa.”


2 bKwa nini mavazi yako ni mekundu,
kama ya yule akanyagaye shinikizo la zabibu?


3 c“Nimekanyaga shinikizo la zabibu peke yangu;
kutoka mataifa hakuna mtu aliyekuwa pamoja nami.
Nimewaponda kwa miguu katika hasira yangu
na kuwakanyaga chini katika ghadhabu yangu;
damu yao ilitia matone kwenye mavazi yangu,
na kutia madoa nguo zangu zote.

4 dKwa kuwa siku ya kisasi ilikuwa moyoni mwangu,
mwaka wa ukombozi wangu umefika.

5 eNilitazama, lakini hakuwepo yeyote wa kunisaidia,
nilishangaa kwa kuwa hakuwepo yeyote aliyetoa msaada;
hivyo mkono wangu wenyewe ndio ulionifanyia wokovu,
na ghadhabu yangu mwenyewe ndiyo iliyonitegemeza.

6 fNilikanyaga mataifa kwa miguu katika hasira yangu,
katika ghadhabu yangu niliwalewesha,
na kumwaga damu yao juu ya ardhi.”
Copyright information for SwhKC